1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Uchumi

Wakenya waonywa kutobadilisha fedha kutumia mitandao haramu

Caro Robi
22 Oktoba 2018

Wakala wa masoko ya fedha nchini Kenya umewaonya wakenya dhidi ya biashara ya ubadilishaji fedha za kigeni kupitia mitandao isiyo na leseni.

https://p.dw.com/p/36w7m
Nairobi Skyline Kenia Stadtansicht
Picha: Fotolia/Natalia Pushchina

Wakala wa masoko ya fedha nchini Kenya -CMA- umewaonya wakenya leo dhidi ya biashara ya kubadilisha fedha za kigeni kupitia mitandao isiyo na leseni. Wakala huo umeonya kwamba kuna hatari ya kupoteza uwekezaji wa fedha zao.

Mkurugenzi mtendaji wa wakala huo Paul Muthaura amesema amegundua watu kadhaa na mitandao mbali mbali wanafanya biashara hiyo ya kubadilisha fedha za kigeni kwa kutumia mitandao ambayo hayajapewa leseni na vyombo vinavyohusika.

Ameongeza kuwa wakala huo wa masoko ya fedha za kigeni unapanga kuchukuwa hatua zinazofaa dhidi ya wanaofanya biashara hiyo kinyume cha sheria.