Waislam waadhimisha Eid al-Fitr
22 Aprili 2023Matangazo
Waislamu kwa mwanzo tofauti jana na leo wanaadhimisha Siku Kuu ya Eid al-Fitr baada ya kumalizika mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.Sikuu Kuu hii kwa mwaka huu imegubikwa na mzozo wa Sudan, huku katika mataifa mengine kukiwa na mashaka ya hatma bora ya baadaye.Baada ya mfungo wa mwezi wa Ramadhani, Waislamu husherehekea Eid al-Fitr na kula pamoja na kukutanisha familia. Kiutamaduni siku hizi zinatokana na kuonekana kwa mwezi mpya, hatua ambayo hutofautiana kulingana na eneo la kijiografia.