1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Viongozi wa NATO kujadili msaada zaidi kwa Ukraine

9 Julai 2024

Viongozi wa nchi za Jumuiya ya kujihami ya NATO wanakutana leo katika mkutano wa kilele wa Jumuiya hiyo unaolenga kuiunga mkono Ukraine dhidi ya Urusi.

https://p.dw.com/p/4i3Q2
NATO / Volodymyr Zelensky na Jens Stoltenberg
Katibu Mkuu wa NATO Jens Stoltenberg na Rais wa Ukraine Volodymyr ZelenskyPicha: Ukrainian Presidency/abaca/picture alliance

Pia mkutano huo utagubikwa na suala la  rais Joe Biden kupambania uhai wake wa  kisiasa. 

Kiongozi huyo wa Marekani anatarajiwa kutumia mkutano huo wa siku tatu wa maadhimisho ya miaka 75 tangu ulipoanzishwa mfungamano huo wa kiulinzi,kuwahakikishia washirika wake juu ya uongozi wa Marekani na uwezo wake wa kuliongoza taifa hilo, wakati miito ikiongezeka ya kumtaka ajiondowe kwenye kinya'ng'anyiro cha kuwania muhula wa pili madarakani.

Soma pia:Mkutano wa kilele wa Ukraine waanza Uswisi lakini huenda ukashindwa kuitenga Urusi

Hata hivyo viongozi wa NATO wanatarajiwa kuonesha bado wanatambuwa hali halisi inayoendelea katika uwanja wa vita nchini Ukraine.

Rais Volodymyr Zelensky nae pia atashiriki mkutano huo wa Washington akiwa na matumani ya kupata msaada wa mifumo zaidi ya ulinzi wa anga aina ya Patriot ambayo, kwa miezi kadhaa amekuwa akiiomba kwa washirika wake.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW