1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaNiger

Niger yakubali pendekezo la Algeria kuwa mpatanishi

2 Oktoba 2023

Wizara ya masuala ya kigeni ya Niger imekubali pendekezo la Algeria kuwa mpatanishi katika mgogoro wake wakisiasa.

https://p.dw.com/p/4X3OH
Kiongozi wa kijeshi wa Niger Jenerali Abdourahamane Tiani akisoma taarifa aliyoitoa kupitia televisheni ya taifa baada ya kuingia madarakani.
Kiongozi wa kijeshi wa Niger Jenerali Abdourahamane Tiani akisoma taarifa aliyoitoa kupitia televisheni ya taifa baada ya kuingia madarakani.Picha: ORTN/Télé Sahel/AFP

Hatua hii inafikiwa wiki tano baada ya taifa hilo la Kaskazini kwa Afrika kupendekeza kipindi cha mpito cha miezi sita nchini Niger kitakachoongozwa na raia.

Wizara hiyo imesema imepokea idhini  rasmi ya ombi la rais Abdelmajid Tebboune wa Algeria la kutaka kuwa mpatanishi. Hadi sasa utawala wa kijeshi wa Niger haujatoa tamko lolote juu ya hatua hiyo.

Algeria mara kwa mara imeonya kuhusu hatua ya uingiliaji kijeshi Niger ambako jeshi lilimpindua rais Mohammed Bazoum mwezi Julai likipendekeza kuwepo miaka mitatu ya kipindi cha mpito.

Mwishoni mwa mwezi Agosti, Waziri wa mambo ya nje wa Algeria Ahmed Attaf alisema taifa hilo limezungumza mara kadhaa na utawala wa kijeshi wa Niger na kupendekeza mkakati wa kuirejesha nchi hiyo katika utawala wa kikatiba.