1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Usalama waimarishwa Uganda Bobi Wine akisubiriwa kurudi

Mohammed Abdulrahman
20 Septemba 2018

Robert Kyagulanyi, maarufu kwa jina la Bobi Wine, anatarajiwa kurudi nyumbani leo kutoka Marekani ambako alikwenda kwa matibabu. Polisi wameanza kuwakamata watu kabla ya mbunge huyo, mkosoaji wa rais Museveni kurejea.

https://p.dw.com/p/35DR6
Uganda Proteste und Ausschreitungen in Kampala
Picha: Getty Images/AFP/I. Kasamani

Polisi nchini Uganda wameanza kuwakamata watu hovyo kabla ya kurejea nyumbani kwa msanii na mbunge mashuhuri wa upinzani, Robert Kyagulanyi, nchini humo hivi leo.

Kyagulanyi, maarufu kwa jina la Bobi Wine, anatarajiwa kurudi nyumbani leo  kutoka Marekani ambako alikwenda kwa matibabu, kutokana na kile alichodai ni kuteswa na maafisa wa usalama alipokuwa rumande.

Polisi wamemkamata ndugu wa mwimbaji huyo na watu wengine wawili wakati wakisafiri kwa gari kuelekea uwanja wa ndege. Wakili Asuman Basalirwa  amesema polisi hawakutoa sababu ya kukamatwa kwao.

Mbunge mwengine wa upinzani Medard Sseggona amesema aliwakimbia polisi waliofika nyumbani kwake  kwa lengo la kumtia nguvuni. Polisi pia waliizingira nyumba ya Meya wa Kampala, Erias Likwago.

Kyagulanyi, mpinzani mkubwa wa Rais Yoweri Museveni, anatarajiwa kuwasili Uganda mchana huu. Polisi wamepiga marufuku mikusanyiko yote ya hadhara.