1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUrusi

Urusi yaishambulia Ukraine kwa droni 12 na kombora

3 Desemba 2023

Urusi imerusha ndege 12 zisizo na rubani na kombora moja la masafa marefu kuelekea Ukraine usiku wa kuamkia leo huku mifumo ya ulinzi wa anga ya Ukraine imeharibu droni 10

https://p.dw.com/p/4Zio7
Droni ya Ukraine inayojulikana kama Punisher ikifanya mazoezi katika eneo la Kyiv mnamo Agosti 11, 2023
Droni ya Ukraine inayojulikana kama PunisherPicha: SERGEI SUPINSKY/AFP

Mashambulizi hayo yameripotiwa na jeshi la anga la Ukraine leo asubuhi lakini hakuna taarifa yoyote iliyotolewa na Moscow.

Ripoti ya jeshi hilo la Ukraine imesema droni zilizorushwa aina ya Shahed zinazotengenezwa nchini Iran, zilikuwa zimeelekezwa Kaskazini Magharibi mwa Ukraine na lakini nyingi ziliangushwa katika eneo la Mykolaiv Kusini mwa Ukraine.

Soma pia:Urusi yaendeleza mashambulizi mashariki mwa Ukraine

Hakukuwa na ripoti za haraka kuhusu uharibifu uliotokana na kuangushwa kwa ndege hizo na nyingine mbili ambazo hazikuharibiwa.

Kuhusu kombora hilo la masafa marefu lililorushwa na Urusi, Ukraine imesema halikuangushwa lakini pia halikufikia shabaha iliyokusudiwa.

Hata hivyo, ripoti ya jeshi hilo haikuweza kuthibitishwa kwa njia huru na pia hakukuwa na tamko la haraka kutoka Urusi.