1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

EU yaidhinisha kurefushwa muda wa vikwazo dhidi ya Urusi

27 Januari 2025

Umoja wa Ulaya umeidhinisha mpango wa kuendeleza vikwazo dhidi ya Urusi kutokana na uvamizi wake nchini Ukraine.

https://p.dw.com/p/4phwb
Ubelgiji, Brussel 2025 | Kaja Kallas
Mkuu wa sera za kigeni wa Umoja wa Ulaya Kaja Kallas.Picha: Nicolas Tucat/AFP/Getty Images

Mawaziri wa mambo ya Nje wa umoja huo walifikia uamuzi huo walipokutana leo mjini Brussels Ubelgiji.

Mkuu wa sera za kigeni wa Umoja wa Ulaya Kaja Kallas amesema hatua hii itaendelea kuinyima Moscow mapato ya kufadhili vita vyake.

SOma pia:Ukraine yaishambulia Urusi kwa droni 121

Hata hivyo kulikuwa na wasiwasi kwamba Hungary ingelipinga hatua hiyo, lakini taarifa zimeeleza kuwa Waziri Mkuu wa Hungary Viktor Orban alifikia makubaliano na wenzake wa Ulaya na kuamua kuunga mkono mpango huo.