1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Umoja wa Ulaya waapa kujibu ushuru wa Marekani

11 Februari 2025

Rais wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Ulaya Ursula von der Leyen ameapa leo kwamba kanda hiyo ya mataifa wanachama 27 itajibu uamuzi wa Marekani wa kuweka ushuru wa asilimia 25 kwa bidhaa za chuma na alumini.

https://p.dw.com/p/4qIbW
Frankreich Paris 2025 | EU-Kommissionspräsidentin von der Leyen beim KI-Gipfel im Grand Palais
Rais wa Tume ya Ulaya Ursula von der Leyen wakati wa mkutano kwenye Grand Palais huko Paris, Ufaransa Februari 11, 2025. Picha: Eliot Blondet/ABACAPRESS.COM/picture alliance

Katika taarifa iliyotolewa na ofisi yake mjini Brussels, Bibi Von der Leyen amesema Umoja wa Ulaya utachukua hatua nzito za kujibu mapigo, akiahidi kwamba kanda hiyo italinda maslahi yake ya kiuchumi dhidi ya kile amekitaja kuwa"ushuru usio na msingi". Rais Donald Trump wa Marekani alitangaza jana Jumatatu ushuru wa asilimia 25 kwa bidhaa zote za chuma na alumini kutoka mataifa ya kigeni akitumai kuyalinda makampuni ya ndani dhidi ya ushindani kutoka nje. Hata hivyo, hatua kama hizo wakati wa utawala wake wa awamu ya kwanza ziliteteresha mahusiano ya Washington na washirika wake na kupandisha bei ya bidhaa za chuma na alumini.