SiasaUkraine
Ukraine yazima shambulizi jingine la Urusi mjini Kyiv
20 Mei 2023Matangazo
Taarifa iliyotolewa na jeshi la anga la Ukraine imesema zaidi ya droni 18 zinazoaminika kuwa zimeundwa nchini Iran zilidunguliwa juu ya anga ya mji wa Kyiv na nyingine 20 ziliangushwa kwenye maeneo tofauti ya Ukraine.
Mamlaka za mji huo mkuu zimesema mabaki yaliyoanguka ya zana hizo za kivita yamesababisha uharibifu wa majengo kadhaa, magari na miundombinu ya barabara lakini hakuna hakuna mtu aliyejeruhiwa wala kupoteza maisha.
Hiyo itakuwa ni mara ya 11 kwa Urusi kuulenga mji wa Kyiv tangu mwanzoni mwa mwezi Mei lakini hujuma hizo hazifanya uharibifu mkubwa kutokana na kuimarika kwa mifumo ya ulinzi ya Ukraine.