1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani kuipa NATO wanajeshi 35,000 kuanzia 2025

12 Oktoba 2023

Waziri wa ulinzi wa Ujerumani Boris Pistorius amesema taifa hilo litaanza kuupatia muungano wa kijeshi wa NATO wanajeshi 35,000 kuanzia mwaka 2025.

https://p.dw.com/p/4XRRg
Boris Pistorius , waziri wa ulinzi wa Ujerumani.
Boris Pistorius , waziri wa ulinzi wa Ujerumani.Picha: Florian Wiegand/Eibner-Pressefoto/picture alliance

Shirika la habari la DPA, limesema tangazo hilo linahusisha mipango mipana iliyoandaliwa na NATO, inayoangazia ulinzi kwenye maeneo yake muhimu na hususan katika, nyakati za dharura.

Pistorius amesema karibu wanajeshi 4,000 wa Ujerumani wanatarajiwa kupelekwa na kubakia Lithuania na kutoa ndege 200 na vifaa vingine muhimu vitakavyopelekwa mara moja.

Mkakati huo unaofanyika katikati ya vita vya Urusi nchini Ukraine, unalenga kuuandaa muungano huo wa kijeshi dhidi ya matukio yoyote makubwa kama ya uvamizi dhidi ya mwanachama wa NATO, ama kutoka Urusi au kundi la kigaidi.