1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUingereza

Starmer aahidi kufufua uhusiano na Ulaya

18 Julai 2024

Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Starmer ameahidi kufufua uhusiano na washirika wa Ulaya ulioharibiwa baada ya Uingereza kujiondoa kutoka Umoja wa Ulaya.

https://p.dw.com/p/4iTVF
Marekani | Mkutano wa NATO | Keir Starmer
Waziri Mkuu wa Uingereza, Keir Starmer ameahidi kuuimarisha uhusiano wake na Ulaya lich ya kujitenga na Umoja wa mataifa ya bara hiloPicha: Evan Vucci/AP Photo/picture alliance

Ametoa mwito wa ushirikiano ili kuendelea kuisaidia Ukraine na kukabiliana na matatizo yanayolikumba bara Ulaya ikiwemo uhamiaji haramu, mabadiliko ya tabianchi na usalama wa nishati.

Akiufungua mkutano wa jumuiya ya kisiasa ya Ulaya EPC ambapo zaidi ya viongozi 40 wanakutana katika kasri la Blenheim, mahali alikozaliwa waziri mkuu wa zamani wa Uingereza Winston Churchill, Starmer ameeleza nia ya kurejesha uhusiano kati ya Uingereza na Ulaya baada ya Brexit.

Kiongozi huyo pia amejitenga na utawala wa serikali iliyopita ambayo ilitishia kujiondoa kwenye mkataba wa kimataifa kuhusu haki za binadamu.