1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais Trump azuia kwa muda uhamiaji Marekani

22 Aprili 2020

Rais wa Marekani Donald Trump amezuia kwa muda uhamiaji nchini Marekani kwa lengo la kuwalinda wafanyakazi wa kimarekani kutokana na msukosuko wa kiuchumi uliosababishwa na janga la virusi vya Corona.

https://p.dw.com/p/3bFgZ
USA Präsident Donald Trump Coronavirus Pressekonferenz
Picha: Getty Images/W. McNamee

Hatua ya Trump imekuja wakati Umoja wa Mataifa umeonya kwamba ulimwengu unakabiliwa na janga kubwa la kibinadamu.

Onyo la Umoja wa Mataifa limetolewa katika kipindi ambacho mataifa ya dunia yanapambana kudhibiti maambukizi ya virusi hivyo ambavyo hadi sasa vimewauwa watu 177,000 na wengine zaidi ya milioni 2.5 wameambukizwa.

Mkurugenzi mtendaji wa shirika la mpango wa chakula la Umoja wa mataifa WFP David Beasley ameliambia baraza la usalama la Umoja wa Mataifa jana kwamba sio tu ulimwengu unakabiliwa na janga la kiafya bali pia janga kubwa la kibinadamu.