Hali ya upungufu wa walimu katika shule za msingi nchini Ujerumani inatarajiwa kuwa mbaya zaidi katika kipindi cha miaka michache inayokuja. Hayo yamefichuliwa kufuatia uchunguzi uliosimamiwa na wakfu wa Bertelsmann na kuchapishwa hivi karibuni. Kwa mujibu wa uchunguzi huo, Ujerumani itapungukiwa na walimu 35,000 ifikapo mwaka 2025.