1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ugiriki yapiga kura, euro mashakani

17 Juni 2012

Wakati Wagiriki wakipiga kura leo (17.06.2012) katika uchaguzi unaoweza kuamua hatima ya taifa hilo katika sarafu ya euro, kushindwa kwa vyama vya kisiasa kutafuta msimamo wa pamoja kunaonyesha hali ya mtafaruku.

https://p.dw.com/p/15Gbl
Greece's Left Coalition party leader Alexis Tsipras, addresses reporters during a joint press conference with France's leftist party Front de Gauche former candidate for the 2012 French presidential elections Jean Luc Melenchon, held at the National Assembly in Paris, Monday May 21, 2012.(Foto:Remy de la Mauviniere/AP/dapd)
Kiongozi wa chama cha Syriza Alexis TsiprasPicha: dapd

Wagombea wakuu, chama cha kihifidhina cha New Democracy na Syriza chama cha nadharia za mrengo wa kushoto, vimeahidi kila kimoja kuunda serikali ambayo itajadili upya masharti magumu ya mkopo wa kuiokoa nchi hiyo uliotolewa na umoja wa Ulaya na shirika la fedha la kimataifa IMF, lakini wanataka kufanya hivyo kwa masharti yao binafsi.

Tatizo ni kwamba kwa mujibu wa uchunguzi wa maoni yaliyopita na kuchapishwa mapema mwezi huu, hakuna chama kitaweza kuongoza bila ya kuwa na washirika , na kuunda hata serikali yenye muungano usio imara ni suala ambalo halina uhakika, wanasema wa wadadisi wa masuala ya kisiasa.

Serikali ya mseto

Iwapo chama cha New Democracy ni chama cha kwanza , uwezekano wa kuunda serikali ya mseto ni rahisi kuliko iwapo chama cha kwanza kitakuwa Syriza, amesema vassiliki Georgiadou, mhadhiri wa sayansi ya kisiasa katika chuo kikuu cha Panteion mjini Athens.

Leader of the conservative New Democracy party Antonis Samaras speaks to his supporters during an election rally at Syntagma square in Athens, Friday, June 15, 2012. Greece faces crucial national elections on Sunday, that could ultimately determine whether the debt-saddled, recession bound country remains in the eurozone. (Foto:Petros Karadjias/AP/dapd)
Kiongozi wa chama cha New Democracy Antonis SamarasPicha: dapd

Lakini hali zote sio rahisi, amesema.

Amesema serikali ya mseto inapaswa kuhusisha vyama vitatu ili kuwa imara, ambapo chama cha Kisoshalist cha Pasok na chama cha Democratic ambacho kinaonekana kuwa kitaweza kuwa chama kitakachotawaza kiongozi wa serikali.

Ameongeza kuwa hali hiyo inatakiwa kuidhinishwa na wapigakura. Serikali yoyote itakumbana na hali ngumu ya kuweka uwiano kati ya matakwa ya umma ya kutaka kupunguzwa kwa hatua za kubana matumzi zilizowekwa katika muda wa miaka miwili iliyopita na msisitizo wa wakopeshaji wa umoja wa Ulaya na shirika la fedha la kimataifa, kuwa Ugiriki ni lazima iendelee na mpango huo.

Msaada wa kimataifa

Ugiriki tayari imelazimika kuomba msaada mara mbili wa uokozi, wa kwanza ukiwa na thamani ya euro bilioni 110 katika mwaka 2010 na tena euro bilioni 130 mwaka huu pamoja na kufutwa kwa deni la watu binafsi lenye thamani ya euro bilioni 107, ikiwa ni jumla ya euro bilioni 347.

epa03222730 MPs of New Democracy conservative party attend a meeting of the party's parliamentary group in the Greek Parliament in Athens, Greece, 17 May 2012. The shortest-lived parliament in Greece's history is due to be dissolved on 18 May by President of the Republic Karolos Papoulias to pave the way for new elections on 17 June 2012. EPA/ORESTIS PANAGIOTOU
Bunge la UgirikiPicha: picture-alliance/dpa

Kiongozi wa chama cha Syriza Alexis Tsipras mwenye umri wa miaka 31 ameahidi kufuta makubaliano ya uokozi na tayari amekataa kushirikiana na chama cha New Democracy ama kile cha Pasok , vyama ambavyo vimeshiriki katika kuiongoza nchi hiyo katika muda wa miongo minne iliyopita.

Karamu ya rushwa

Tspras amevishutumu vyama vyote viwili kwa kuitumbukiza nchi hiyo katika kile alichokieleza kuwa ni hafla ya rushwa, katika miaka vilivyokuwa madarakani na ameahidi kukomesha mfumo huo wa uoza.

Antonio Samaras mwenye umri wa miaka 61 ,ambaye ni mkubwa wake kiumri , amebeua ahadi za chama cha Syriza za kurejesha mishahara kama zamani, kuwa ni uchumi wa vitabu vya vichekesho.

Umma, pamoja na hali halisi vinadai kuwa serikali ni lazima iundwe. Haiwezekani kuendelea zaidi zaidi ya hapa, amesema kiongozi wa chama cha New Democracy Samaras hapo kabla.

Wakati huo huo mkuu wa shirika la ushirikiano wa kiuchumi na maendeleo katika bara la Ulaya OECD, Angel Gurria amesema kuwa Ugiriki inapaswa kupewa nafasi ya kujadili upya masharti ya mpango wa kimataifa wa uokozi wenye thamani ya euro bilioni 130, iwapo hii itakuwa na maana ya kuibakisha nchi hiyo katika eneo linalotumia sarafu ya euro.

Mwandishi : Sekione Kitojo / afpe / rtre

Mhariri : Sudi Mnette