1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUgiriki

Ugiriki yaingia katika duru ya pili ya uchaguzi

25 Juni 2023

Raia wa Ugiriki wanapiga kura leo Jumapili katika uchaguzi mkuu wa pili kufanyika ndani ya wiki tano.

https://p.dw.com/p/4T2GI
Griechenland | Parlamentswahlen | Stimmabgabe
Picha: Louiza Vradi/REUTERS

Katika uchaguzi huu, Waziri mkuu Kyriakos Mitsotakis anatafuta kutetea kiti chake kwa muhula wa pili kupitia chama chake cha kihafidhina cha New Democracy (ND).

Soma Pia: Wahafidhina washinda uchaguzi nchini Ugiriki

Kwenye uchaguzi wa awali uliofanyika mwezi Mei, Mitsotakis alipata ushindi mkubwa lakini alikosa viti vitano vya wabunge ambavyo vingemuwezesha kuanzisha na serikali thabiti ya chama kimoja.

Licha ya kuwaomba wafuasi wake wajitokeze kwa wingi kwenye uchaguzi wa leo, Waziri huyo mkuu wa Ugiriki ametahadharisha kuwepo kwa uwezekano wa kufanyika kwa uchaguzi kwa mara ya tatu ikiwa atashindwa kupata kura za kutosha na viti vingi zaidi bungeni.

Mpinzani mkubwa wa Mitsotakis ni Waziri mkuu wa zamani  Alexis Tsipras, aliyeshika nafasi ya pili katika uchaguzi wa mwezi Mei.