1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Uganda yajitenga na msimamo wa Sebutinde katika ICJ

28 Januari 2024

Uganda imejitenga na maoni yaliyoandikwa na jaji wa nchini humo Julia Sebutinde ya kupinga uamuzi uliotolewa na Mahakama ya Kimataifa ya Haki ICJ katika dhidi ya Israel.

https://p.dw.com/p/4blek
The Hague
Majaji katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) wakati wa uamuzi wa keshi iliyowasilishwa na Afrika Kusini dhidi ya Israel.Picha: Piroschka van de Wouw/REUTERS

Serikali ya Uganda kupitia taarifa yake imesema kwamba msimamo uliochukuliwa na Jaji Sebutinde ni wake binafsi, na hauakisi kwa njia yoyote  nafasi ya serikali ya Jamhuri ya Uganda.

Soma pia: ICJ yatambua hatari ya kimbari Ukanda wa Gaza

Aidha iliongeza kuwa nchi hiyo ya Afrika Mashariki inaunga mkono msimamo wa vuguvugu la mataifa yasiyofungamana na upande wowote kwenye mzozo huo, uliopitishwa katika mkutano mkuu uliofanyika katika mji mkuu Kampala mwezi huu.

Sebutinde ni moja kati ya majaji wawili kwenye jopo la wanachama 17 waliopiga kura ya kupinga hatua zilizopitishwa na mahakama ya ICJ katika kuiamuru Israeli kuchukua hatua kuzuia vitendo vya mauaji ya halaiki wakati ikipambana na wanamgambo wa Hamas katika Ukanda wa Gaza.