1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ufaransa yapeleka wanajeshi zaidi Mali

15 Januari 2013

Ufaransa imeendelea na mashambulio yake ya anga dhidi ya maeneo yanayoshikiliwa na waasi nchini Mali,wakati mipango ya kuweka jeshi la Afrika ikiwa mbioni, huku kukiwa na wasiwasi kuhusu ucheleweshaji wa jeshi hilo.

https://p.dw.com/p/17K8b
French soldiers walk past a hangar they are staying at the Malian army air base in Bamako January 14, 2013. France plans to increase its troops in Mali to 2,500 in the days ahead and is working to speed up the deployment of West African troops for a campaign against Islamist rebels, the government said on Monday. REUTERS/Joe Penney (MALI - Tags: CONFLICT MILITARY POLITICS)
Majeshi ya Ufaransa yakijitayarisha mjini BamakoPicha: Reuters

Wakati huo huo, rais wa Ufaransa, Francois Hollande, yuko katika ziara ya siku moja katika Umoja wa Falme za Kiarabu akiyataka mataifa ya Kiarabu kusaidia katika juhudi za kupambana na waasi wa Kiislamu nchini Mali.

Ufaransa tayari imekwishapeleka mamia ya wanajeshi wake nchini Mali na inatarajia kutuma wanajeshi zaidi baada ya kufanya mashambulizi ya anga kwa siku kadhaa tangu Ijumaa iliyopita katika eneo kubwa la jangwa lililokamatwa mwaka jana na muungano wa makundi ya Kiislamu ambayo yanajumuisha pia tawi la kundi la al-Qaeda katika mataifa ya Afrika kaskazini pamoja na kundi la MUJWA linalotokea nchini Mali, pamoja na kundi la Ansar Dine.

French President Francois Hollande delivers his speech as he attends New Year wishes ceremony for diplomats at the Elysee Palace in Paris, January 11, 2013. REUTERS/Philippe Wojazer (FRANCE - Tags: POLITICS)
rais wa Ufaransa Francois HollandePicha: Reuters

Akizungumza kutoka katika kituo cha kijeshi cha Ufaransa mjini Abu Dhabi mwanzoni mwa ziara yake ya siku moja katika Umoja wa falme za Kiarabu, rais Francois Hollande amesema majeshi ya Ufaransa nchini Mali yamefanya mashambulio zaidi usiku wa jana, ambayo yamefanikiwa kushambulia mahali palipokusudiwa.

A French Rafale fighter jet lands in Ndjamena, Chad, before being deployed in Mali, in this picture provided by the French Military Communications Audiovisual office (ECPAD) and taken on January 13, 2013. Al Qaeda-linked Islamist rebels in Mali launched a counter-offensive on Monday after three days of strikes by French fighter jets on their strongholds in the desert north, vowing to drag France into a long and brutal ground war. Photo taken January 13, 2013. Mandatory Credit. REUTERS/Adj. Nicolas-Nelson Richard/ECPAD/Handout (FRANCE - Tags: MILITARY POLITICS TRANSPORT) ATTENTION EDITORS - THIS IMAGE WAS PROVIDED BY A THIRD PARTY THIS PICTURE IS DISTRIBUTED EXACTLY AS RECEIVED BY REUTERS AS A SERVICE TO CLIENTS. NO SALES. NO ARCHIVES. FOR EDITORIAL USE ONLY. NOT FOR SALE FOR MARKETING OR ADVERTISING CAMPAIGNS. THIS IMAGE HAS BEEN SUPPLIED BY A THIRD PARTY. IT IS DISTRIBUTED, EXACTLY AS RECEIVED BY REUTERS, AS A SERVICE TO CLIENTS. MANDATORY CREDIT
Ndege za kijeshi za Ufaransa zikiruka kuendelea na mashambuliziPicha: Reuters

Ufaransa inakusudia kuweka jumla ya wanajeshi 2,500 katika koloni lake hilo la zamani kuimarisha jeshi la Mali pamoja na kufanya kazi kwa pamoja na jeshi linaloingilia kati, lililotolewa na mataifa ya Afrika magharibi ya jumuiya ya ECOWAS.

Waziri wa mambo ya kigeni wa Ufaransa anayeongozana na rais na Hollande katika ziara hiyo ambayo ina lengo la kuimarisha mahusiano ya kibiashara na kuwezesha kupiga hatua katika uwezekano wa mauzo ya ndege 60 za kijeshi chapa Rafale, amesema kuwa ana imani mataifa ya Kiarabu ya eneo la ghuba pia yatasaidia kampeni inayofanyika nchini Mali.

Waziri wa mambo ya kigeni wa Ujerumani, Guido Westerwelle, amesema Ujerumani haitashiriki katika kupeleka jeshi nchini Mali lakini itasaidia katika masuala ya kimbinu.

"Inawezekana baadaye tukasaidia usafirishaji wa majeshi, na pia kutoa msaada wa kimbinu, kisiasa, kiutu ama dawa kwa majirani zetu Ufaransa na marafiki zetu".

Bundesaußenminister Guido Westerwelle (FDP) spricht am 04.12.2012 in Bad Krozingen (Baden-Württemberg) bei der Eröffnung des Walter-Scheel-Forums. Westerwelle hielt einen Grundsatzvortrag zu den deutsch-russischen Beziehungen. Foto: Patrick Seeger/dpa +++(c) dpa - Bildfunk+++
Waziri wa mambo ya kigeni wa Ujerumani Guido WesterwellePicha: picture-alliance/dpa

Akijibu swali kutoka kwa waandishi habari katika ziara ya Umoja wa falme za Kiarabu, waziri wa mambo ya kigeni wa Ufaransa, Laurent Fabius, ameongeza kuwa kuwapo majeshi ya Ufaransa katika nchi ambayo ni ya Kiislamu katika bara la Afrika hakutaongeza nguvu za kundi la al-Qaeda kupata wafuasi zaidi kutoka katika eneo hilo.

Wakati huo huo, wapiganaji wa kundi la Taliban nchini Afghanistan wameshutumu leo jeshi la Ufaransa kuingilia kati mzozo wa Mali, likionya kuwa hatua hiyo itakuwa na matokeo mabaya. Taliban imesema katika tovuti yake kuwa Ufaransa inapaswa kujifunza kutokana na kushindwa kwa vita nchini Afghanistan na Iraq.

Mataifa ya magharibi pamoja na mataifa jirani yana hofu kuwa wapiganaji wa Mali wataitumia ardhi ya nchi hiyo kama sehemu ya kufanyia mashambulizi yao dhidi ya mataifa ya kigeni.

Mwandishi : Sekione Kitojo / afpe / rtre

Mhariri:Josephat Charo