1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaSudan

Sudan yatishiwa na maandamano mapya

31 Januari 2023

Waandamanaji wanapanga kuandamana kote nchini Sudan kulitaka jeshi la nchi hiyo kukabidhi madaraka kwa mamlaka za kiraia, baada ya mapinduzi ya mwaka 2021 kukwamisha mchakato wa mpito kuelekea demokrasia.

https://p.dw.com/p/4MuMI
Proteste im Sudan
Picha: Marwan Ali/AP Photo/picture alliance

Vikosi vya usalama vimeendesha ukandamizaji dhidi ya maandamano kama hayo tangu jeshi lilipotwaa madaraka, na kuuwa watu wasiopungua 100, kwa mujibu wa chama cha madaktari kinachoegemea makundi ya kudai demokrasia. Katika mji mkuu Khartoum, waandamanaji watajaribu kuandamana kuelekea kasri ya rais ambako wana uhakika wa kukumbana na askari polisi waliojihami pakubwa. Na kama ilivyoshuhudiwa katika maandamano mengine, mamlaka huenda zikayafunga madaraja mjini Khartoum ili kuzuwia waandamanaji kukusanyika. Maandamano ya kudai demokrasia yameendelea nchini Sudan licha ya makubaliano ya Desemba kati ya jeshi la makundi ya upinzani ya kiraia kukomesha mzozo wa kisiasa wa taifa hilo.