1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaBurundi

Shambulizi la waasi lasababisha vifo vya watu 20 Burundi

24 Desemba 2023

Shambulizi la waasi Magharibi mwa Burundi limesababisha vifo vya watu 20 wote wakiwa raia

https://p.dw.com/p/4aWzl
Symbolbild I Soldaten Burundi
Picha: STR/AFP/Getty Images

Kundi la waasi wa RED-Tabara limekiri kuhusika katika shambulizi hilo, na kulingana na taarifa yake, limewauwa wanajeshi 10.

Shambulizi hilo lilitokea jana jioni katika mji wa Vugizo karibu na mpaka kati ya nchi hiyo na Jamhuri ya kidemokrasi ya Kongo, ambako waasi wameweka ngome yao.