1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

SEOUL : Korea Kaskazini kurudi katika mazungumzo

22 Februari 2005
https://p.dw.com/p/CFbz

Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-il amemweleza mjumbe wa China kwamba nchi yake itarejea kwenye mazungumzo ya nuklea ya nchi sita iwapo mazingira ya kufanya hivyo yatakuwa sahihi na Marekani kuonyesha uaminifu.

Hiyo ni taarifa ya kwanza kutolewa na kiongozi huyo tokea Korea Kaskazini kutangaza hadharani kwa mara ya kwanza mwezi huu kwamba ina silaha za nuklea na inajitowa kwenye mazungumzo yenye kuzishirikisha Korea Kusini,China,Russia,Marekani na Japani juu ya mpango wake wa nuklea.

Shirika la habari la serikali nchini Korea Kaskazini la KCNA limemkariri Kim akimwambia Wang Jiarui mkuu wa idara ya ushirikiano ya Chama cha Kikomunisti cha China kwamba watakwenda kwenye meza ya mazungumzo wakati wowote ule iwapo kutakuwepo na mazingira yaliyokomaa kwa ajili ya mazungumzo hayo kutokana na juhudi za pamoja za nchi husika kwa ajili ya kipindi cha usoni.