1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Sekretarieti ya EAC yawasilisha makadirio ya bajeti yake

14 Juni 2023

Jumuiya ya Afrika Mashariki imewasilisha Makadirio ya bajeti kwa bunge la Jumuiya hiyo ambayo ni dola za kimarekani zaidi ya milioni miamoja na tatu, kwa mwaka wa fedha 2023-2024.

https://p.dw.com/p/4SY4N
Logo Ostafrikanische Gemeinschaft EAC

Katika hotuba yake ya uwasilishwaji wa bajeti, mwenyekiti wa mawaziri wa jumuiya hiyo Ezechiel Nibigira  raia wa Burundi, amebainisha kwamba makadirio ya bajeti ya mwaka huu yanawasilishwa wakati uchumi wa jumuiya hiyo kongwe barani Afrika,  ukiwa mashakani kutokana na misukosuko ya kimataifa ikiwapo vita na mabadiliko ya tabia nchi. 

Hotuba hiyo iliyosomwa katika makao makuu ya  jumuiya ya Afrika Mashariki  Arusha Tanzania pia ilibainisha kwamba  pamoja na changamoto hizo, lakini  ukuaji wa uchumi katika ukanda huo uliimarika kwa asilimia 4. 8 mwaka 2022, kutoka asilimia 3.5 mwaka 2021.

Bajeti hiyo imezingatia maeneo tisa ya vipaumbele, ikiwapo uimarishaji wa michakato ya utawala wa kikanda, uboreshaji wa mifumo ya forodha pamoja na usimamizi wa mifumo ya amani ya kikanda na kimataifa.