1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Scholz akwepa kumtaja wanaemuunga mkono Umoja wa Ulaya

11 Juni 2024

Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz amekwepa kutamka kuwa atamuunga mkono Rais wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Ulaya, Ursula von der Leyen katika ombi lake la kuwania muhula mwingine wa kiti hicho.

https://p.dw.com/p/4gt5x
Ubelgiji Brussels | Ursula von der Leyen
Rais wa Halmashauri Kuu ya Ulaya Ursula von der Leyen akizungumza wakati wa hafla siku ya uchaguzi wa Bunge la Ulaya huko Brussels, Ubelgiji, Juni 9, 2024. Picha: Piroschka van de Wouw/REUTERS

Hayo yametokea siku moja tu, baada ya uchaguzi wa bunge la Umoja wa Ulaya. Scholz alirudia msimamo wake wa awali kwamba urais wa kamisheni lazima uwe na uungawaji mkono wa msingi wa wingi wa kidemokrasia wa kijadi katika Bunge la Ulaya. Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari mjini Berlin akiwa na Rais wa Chile anayezuru nchini Ujerumani, Gabriel Boric, Scholz amesema, hata hivyo upo uwezekano wa kuzingatia kumuunga mkono sambamba nawagombea mbalimbali wa nafasi za juu za Umoja wa Ulaya katika majuma yajayo.Von der Leyen, mwanasiasa wa Ujerumani na waziri wa zamani kutoka chama cha kihafidhina cha Conservative Christian Democrats (CDU), alitoa wito kwa vyama vya kidemokrasia na vya kiliberali vya Umoja wa Ulaya kuunga mkono azma yake ya kuwania tena kiti cha halmashauri kuu ya umoja huo.