1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Saudia kuitambua Israel iwapo mzozo wa Gaza utasuluhishwa

16 Januari 2024

Waziri wa mambo ya nje wa Saudi Arabia amesema utawala huo wa kifalme unaweza kuitambua Israel iwapo makubaliano ya kina yatafikiwa juu ya mzozo wa Palestina ikiwa ni pamoja na kuitambua Palestina kama taifa huru.

https://p.dw.com/p/4bKaD
Südafrika BRICS Gipfel Saudi-Arabien Faisal bin Farhan Al Saud
Picha: MARCO LONGARI/AFP

Mwanamfalme Faisal bin Farhan amesema, wanakubali kuwa amani ya kikanda inajumuisha pia amani kwa Israel japo hilo linaweza kutokea kupitia kuitambua Palestina kama taifa.

Alipoulizwa wakati wa kongamano la kiuchumi la dunia linalofanyika Davos iwapo Saudi Arabia inaweza kuitambua Israel kama sehemu ya makubaliano mapana ya kisiasa, mwanamfalme huyo alijibu, "Hakika."

Waziri huyo wa mambo ya nje ya Saudi Arabia ameeleza kuwa, suala la kupatikana kwa amani ya kikanda kupitia uundwaji wa taifa la Palestina ni "jambo ambalo wamekuwa wakilifanyia kazi na utawala wa Marekani" na kwamba limekuwa muhimu zaidi wakati huu kwa kuzingatia kinachoendelea katika ukanda wa Gaza.