1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rwanda: Binti akamatwa kwa kuvaa nguo isiyo ya 'heshima‘

Lillian Mtono19 Agosti 2022

Binti mmoja mwenye umri wa miaka 24 raia wa Rwanda, Liliane Mugabekazi anakabiliwa na kifungo cha hadi miaka miwili jela kwa madai ya kuvaa nguo isiyo ya 'heshima'.

https://p.dw.com/p/4Fm9V

Anadaiwa kuvaa nguo hiyo 'isiyo ya heshima' alipohudhuria tamasha la msanii maarufu kutoka nchini Ufaransa, Agosti 7.

Kulingana na mwendesha mashitaka wa serikali Liliane, alivaa nguo zilizokuwa zikionyesha sehemu zake za siri.

Hatua aliyosema iliashiria ukiukaji wa maadili na tamaduni. Hatua ya kukamatwa kwake imeibua mjadala mkubwa nchini humo. Ili kujua zaidi, Lilian Mtono amezungumza na mwenzetu aliyeko mjini Kigali, Janvier Popote na kwanza amemuuliza mjadala mkuu ni upi?