1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais wa zamani wa UEFA Johansson afariki

Sekione Kitojo
5 Juni 2019

rais wa zamani wa shirikisho la kandanda barani Ulaya Lennart Johansson kutoka Sweden amefariki dunia leo(05.06.2019) mjini Stockholm. Johansson atakumbukwa kuwa ni baba wa Champions League barani Ulaya.

https://p.dw.com/p/3JtGj
Lennart Johansson
Picha: PA/dpa

Lennart Johansson , rais  wa  zamani  wa shirikishio la  kandanda  barani Ulaya  UEFA  anayeangaliwa  kama  baba  wa  mashindano  ya  Champions League  katika  bara  hilo, amefariki dunia akiwa  na  umri  wa  miaka 89, shirikisho  la  kandanda  nchini  Sweden  limesema leo Jumatano. "Soka nchini  Sweden  linaomboleza," shirikisho  la  soka  nchini  humo  limesema.

Lennart Johansson
Rais wa zamani wa UEFA Lennart Johansson Picha: Imago Images/Bildbyran/A.L. Eriksson

Kipindi  cha  uongozi  wa  Johansson  katika  shirikisho  la  kandanda  barani Ulaya  UEFA, kuanzia  mwaka  1990  hadi  2007, uliingiliana  na  kuzaliwa kwa  Champions League, mashindano  makubwa  kabisa  duniani  ya  vilabu, na mabadiliko  makubwa  ya  kandanda  kuwa  biashara  kubwa  dunia kwa kuwa  na  mvuto  mkubwa  na  mapato yaliyoelekezwa  na  mapato  kutokana na  televisheni.

Tangazo  la  kifo  chake  Johansson , akiwa  kipenzi cha  wengi  licha  ya  sifa yake  ya  mtu  asiyependa  mchezo, limekuja  muda  mfupi tu kabla  ya ufunguzi wa  mkutano  mkuu  wa  FIFA  mjini  Paris  ambako  wajumbe  ikiwa ni  pamoja  na  rais Gianni Infantino walikaa  kimya  kwa  muda  wa  dakika moja  kumkumbuka.

Mtu wa  mfano

"Nimevunjika  moyo kutokana  na  taarifa  hizi  za  kuondokewa  na  Lennart Johansson," Infantino  amesema  taarifa. alikuwa  raifiki  na kisima  cha hekima  kubwa  na hamasa. Nitamshukuru  milele  kwa  kuwa  nae  akiwa  rais wa  UEFA  wakati  ninajiunga  na  shirikisho  hilo  mwaka  2000.

FIFA und UEFA Sepp Blatter und Lennart Johansson
Lennart Johansson (kulia ) akiwa na rais wa zamani wa FIFA Sepp Blatter(kushoto)Picha: AP

"Tangu  wakati  huo , Lennart  amekuwa  wakati  wote  mtu  wa  mfano wa utendaji  wa weledi na muhimu  zaidi , kwa  utu."

Rais  wa  UEFA Aleksander Ceferin  amesema  mtangulizi  wake  alikuwa "mtumishi  wa  kandanda" ambaye  atakumbukwa  daima  kama "msanifu  wa UEFA  Champions League". Johansson  alionekana  mara  ya  mwisho hadharani  katika  fainali  ya  ligi  ya  Ulaya  kati  ya  Chelsea  na  Arsenal  mjini Baku Mei 29. Alitarajiwa  katika  fainali  ya Champions League  kati  ya Liverpool  na Tottenham Hotspur Juni 1, mjini  Madrid lakini  hakuweza kuhudhuria.

Alizaliwa  Novemba  5, 1929 katika  familia  ya  kawaida  mjini  Stockholm katika  kitongoji cha  Bromma, Johansson alipanda ngazi  kuanzia  akiwa mhudumu  kwa  mkurugenzi wa  kampuni  ya  ujenzi. Alianza kuwa  kiongozi wa  masuala  ya  mpira  wa  miguu  katika  miaka  ya  1960, akiwa  rais wa klabu  kubwa  ya  Sweden ya  AIK, na  kisha  kuwa  mkuu  wa  shirikisho  la kandanda  la  Sweden  kabla  ya  kuchaguliwa  kuwa  mkuu  wa  UEFA mwaka 1990.