1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais wa Poland aitaka Ujerumani iwalipe fidia ya vita

1 Septemba 2024

Rais wa Poland Andrzej Duda kwa mara nyigine ameitaka Ujerumani iilipe fidia nchi yake kwa uharibifu iliyoupitia wakati wa Vita Vikuu vya Pili vya Dunia.

https://p.dw.com/p/4k9LE
Maadhimisho ya miaka 85 tangu kuzuka kwa Vita vya pili  vya dunia Poland
Rais wa Jamhuri ya Poland Andrzej Duda akiweka maua mbele ya kumbukumbu ya waathiriwa wa shambulio la mabomu la Ujerumani tukio lililotokea Septemba 1, 1939, huko Wieluñ, Poland. Picha: Marian Zubrzycki/PAP/dpa/picture alliance

Rais Duda amerejelea madai hayo leo katika hotuba yake ya maadhimisho ya kumbukumbu ya miaka 85 tangu Ujerumani chini ya utawala wa manazi  ilipoivamia Poland.

Akizungumza katika mji mdogo wa Wielu uliokuwa wakati huo karibu na mpaka kati ya Ujerumani na Poland, Duda amesema suala la kusamehe na kukiri makosa ni kitu kimoja lakini kulipa fidia ni suala jingine.Duda ni miongoni mwa viongozi wa ngazi za  juu wa chama cha kihafidhina PiS kilichowahi kuiongoza seriikali.

Wakati huo serikali ya PiS ilikuwa na mahusiano mabaya na Ujerumani ambapo Poland iliishinikiza Ujerumani iilipe fidia ya jumla ya Euro Trilioni 1.3. Serikali ya sasa inayoongozwa na waziri mkuu Donald Tusk ambayo ina maelewano na serikali ya mjini Berlin,iko kwenye mazungumzo na Ujerumani yaliyoanza mwezi Julai,juu ya suala hilo la fidia.