1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais wa Iran kumtembelea Mfalme wa Saudi Arabia

20 Machi 2023

Rais wa Iran Ebrahim Raisi ameukaribisha mualiko kutoka kwa Mfalme Salman wa Saudi Arabia wa kuitembelea nchi hiyo.

https://p.dw.com/p/4OvF9
Ebrahim Raisi | iranischer Präsident
Picha: Iranian Presidency Office/APAimages/IMAGO

Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Iran Hossein Amirabdollahian amesema kuwa Tehran imependekeza sehemu tatu za kufanyika mkutano na mwenzake wa Saudia.

Iran na Saudi Arabia zilikubaliana kurejesha mahusiano na kuzinfungua balozi zao mnamo Machi 10 mwaka jana katika muafaka uliosimamiwa na China.

Soma pia: Nchi kadhaa zasifu hatua ya Iran na Saudia kufufua uhusiano

Nchi hizo mbili kwa miaka mingi zimekuwa zikigombea ushawishi katika Mashariki ya Kati, kwa kuunga mkono makundi pinzani katika vita vya nchini Yemen na Syria.

Wakati huo huo, Iraq na Iran zimesaini makubaliano ya kuimarisha usalama wa mpakani. Makubaliano hayo yalitangazwa jana na ofisi ya Waziri Mkuu wa Iraq na Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran.