1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais Museveni avunja kimya chake kuhusu maandamano mjini Kampala.

Jane Nyingi/ AFPE..Picha AFP15 Septemba 2009

Rais wa Uganda Yoweri Museveni ameapa kuwachukua hatua kali waandamanaji waliotiwa mbaroni wiki iliyopita kufuatia maandamano mjini Kampala yaliyosababisha vifo vya watu 14.

https://p.dw.com/p/JhJU
Raais Yoweri Museveni wa Uganda.Picha: AP

Rais Museveni alisema hayo bungeni kufuatia kikao maalum alichoitisha kuzungumzia kuhusu maandamano hayo Karibu watu 600 walitiwa mbaroni na zaidi ya 200 kati yao kufunguliwa mashtaka,kufuatia maandmano yaliyochochewa na hatua ya serikali kumzuia mfalme wa Wabaganda Ronal Muwenda Mutebi wa pili kuzuru kaskazini mashariki mwa mji wa Kampala mwishoni mwa wiki iliyopita.Hivi punde nimezungumza na mwandishi wetu wa mjini Kampala leila Ndinda na kwanza anaelezea kilichokuwemo katika hotuba hiyo ya rais Museveni aliyotagazwa kwa taifa