1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais Macron wa Ufaransa akataa ombi la Waziri Mkuu kujiuzulu

8 Julai 2024

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amekataa ombi la Waziri Mkuu Gabriel Attal kujiuzulu na kumtaka kuendelea na majukumu yake kwa lengo la kuhakikisha utulivu wa nchi hiyo.

https://p.dw.com/p/4i1fl
Emmanuel Macron
Rais wa Ufaransa Emmanuel MacronPicha: Ludovic Marin/AFP/Getty Images

Attal alitanagza dhamira ya kuwasilisha barua yake ya kujiuzulu kufuatia matokeo ya duru ya pili ya uchaguzi wa Bunge, ambao haujatoa mshindi wa moja kwa moja atakayelidhibiti Bunge la Ufaransa.

Hata hivyo kwenye uchaguzi huo wa jana muungano wa siasa za mrengo wa kushoto wa New Popular Front (NPF) ndio umepata idadi kubwa ya viti kulivyo vyama vingine.

Muungano wa vyama vya mrengo wa kushoto washinda duru ya pili ya uchaguzi Ufaransa

Kufuatia matokeo hayo Attal anayetoka upande wa rais Macro alitangaza mpango wa kujiuzulu lakini akasema atasalia mamlakani ikiwa itahitajika. Kuondoka kwake kungeiacha Ufaransa bila kiongozi wa serikali ikiwa zimesalia wiki tatu kabla ya kuanza kwa Michezo ya Olimpiki mjini Paris.

Urusi imesema haina matumaini yoyote ya kuimarika kwa mahusiano yake na Ufaransa kufuatia ushindi huu wa muungano wa mrengo wa kushoto katika uchaguzi wa Bunge.