1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Uchaguzi mkuu wa Uhispania unafanyika leo

23 Julai 2023

Wapiga kura nchini Uhispania wameanza kupiga kura leo katika uchaguzi mkuu ambao unaweza kushuhudia taifa hilo kuwa mwanachama wa hivi karibuni wa Umoja wa Ulaya kuelekea katika siasa za Kihafidhina.

https://p.dw.com/p/4UHT6
Waziri Mkuu wa Uhispania Pedro Sanchez akishiriki kupiga kura
Waziri Mkuu wa Uhispania Pedro Sanchez akishiriki kupiga kura Picha: Emilio Morenatti/AP/picture alliance

Waziri Mkuu Pedro Sanchez aliitisha uchaguzi wa mapema, baada ya chama chake cha Kisosholisti na mshirika wake chama cha Unidas Podemos, kuanguka katika uchaguzi wa serikali za mitaa mnamo mwezi Mei. Sanchez amekuwa Waziri Mkuu wa Uhispania tangu mwaka 2018.

Soma zaidi: Uhispania yafanya uchaguzi muhimu wa serikali za mitaa

Utafiti mwingi wa kura za maoni kuhusu uchaguzi wa leo unakiweka chama cha Kihafidhina cha People's Party ambacho kilishinda uchaguzi wa Mei, mbele ya Wasosholisti, lakini kitahitaji uungwaji mkono wa chama chenye mrengo mkali wa kulia cha Vox Party ikiwa watatakiwa kuunda serikali mpya.