1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Qatar kuongeza uzalishaji wa gesi asilia ya kimiminika

Sylvia Mwehozi
25 Februari 2024

Qatar itaongeza uzalishaji wa gesi licha ya kushuka kwa kasi kwa bei ya gesi duniani, ikisonga mbele na mipango ya kuchimba zaidi rasilimali hiyo huku kukiwa na ushindani mkali na wapinzani kama vile Marekani.

https://p.dw.com/p/4crlu
Qatar | mji wa kiviwanda wa Ras Laffan
Picha inaonyesha Jiji la Viwanda la Ras Laffan, eneo kuu la Qatar kwa ajili ya uzalishaji wa gesi ya kimiminika kaskazini mwa mji mkuu wa Doha.Picha: Karim Jaafar/AFP/Getty Images

Qatar itaongeza uzalishaji wa gesi licha ya kushuka kwa kasi kwa bei ya gesi duniani, ikisonga mbele na mipango ya kuchimba zaidi rasilimali hiyo huku kukiwa na ushindani mkali na wapinzani kama vile Marekani.

Mkuu wa shirika la nishati la Qatar, Saad al-Kaabi ametangaza hii leo juu ya upanuzi mpya wa uzalishaji wa gesi asilia ya kimiminika ambao utaongeza tani milioni 16 kwa mwaka.

Soma: Umoja wa Falme za Kiarabu wakubali kusambaza gesi na dizeli nchini Ujerumani

Tangazo la Qatar linatolewa wakati bei ya biashara ya gesi ya Marekani ikiporomoka baada ya muongo mmoja wa kupanda kwa uzalishaji ambao uliifanya Washington kuwa miongoni mwa wauzaji wa juu wa mafuta na gesi nje ya nchi.

Bei ya gesi barani Ulaya pia iliporomoka kwa kasi baada ya kushuka kwa usambazaji wa Urusi licha ya Marekani na Qatar kusaidia kuzipa pengo la kiasi kilichopotea.