1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Putin kukutana na Jinping

Josephat Charo
17 Oktoba 2023

Rais Vladimir Putin wa Urusi amewasili nchini China kukutana na mwenyeji wake Rais Xi Jinping kuimarisha uhusiano wao wakati akishiriki katika mkutano wa kilele uliogubikwa na vita baina ya Israel na Hamas.

https://p.dw.com/p/4XcT6
China Peking | Gipfeltreffen Seidenstraße | Putin
Rais Vladimir Putin wa Urusi (katikati) akiwasili mjini Beijing, China, kuhudhuria mkutano wa kilele wa Mradi wa Madaraja na Barabara wa China.Picha: Kyodo/IMAGO

China inawaalika wawakilishi wa nchi 130 kuhudhuria mkutano kuhusu mradi mkubwa wa biashara na miundombinu wa Rais Xi.

Ikulu ya Kremlin ilisema Rais Putin angelifanya mazunguzo na Xi kandoni mwa mkutano huo wa Jumatano (Oktoba 18), utakaojikita juu ya masuala ya kimataifa na kikanda.

Soma zaidi: Putin akubali pendekezo la China kwa mzozo wa Ukraine

Siku ya Jumanne (Oktoba 17) Xi aliufungua mkutano wa Beijing kwa kufanya mazungumzo na Rais Gabriel Boric wa Chile na Rais Kassym-Jomart Tokayev wa Kazakhstan.

Baadaye alikutana na Waziri Mkuu wa Hungary Viktor Orban akimueleza kama rafiki na kumshukuru kwa kuunga mkono mradi wa biashara na miundombinu wa China.

Xi pia alikutana na mawaziri wakuu wa Ethiopia na Papua New Guinea.