1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Papa Francis ateuwa makadinali wapya 21

30 Septemba 2023

Papa Francis leo hii amepandisha hadhi makasisi 21 kutoka pembe zote za dunia hadi cheo cha ukadinali, ambao wengi wao huenda siku moja wakapiga kura kumchagua mrithi wake.

https://p.dw.com/p/4WzmI
Vatikan | Neue Kardinäle
Picha: Riccardo De Luca/AP Photo/picture alliance

Uchaguzi wa "Wakuu wa Kanisa" wapya, ambao ni pamoja na wanadiplomasia, washauri wa karibu na wasimamizi, unatazamwa kwa karibu kama dalili ya mwelekeo wa baadaye wa Kanisa Katoliki.Mmoja wao pia anaweza kuwa mrithi wa Papa Francis mwenye umri wa miaka 86, ambaye huenda akajiuzulu mapema, ingawa yeye mwenyewe anasema bado hajafikiria hatua hiyo.Hafla hiyo ya Jumamosi hii ambayo inafahamika kama kama Baraza la Makadinali, ni ya tisa tangu Papa Francis achaguliwe kuwa papa na wenzake mwana 2013.