1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaPakistan

Polisi ya Pakistan yapambana na wafuasi wa Khan

11 Februari 2024

Polisi nchini Pakistan imepambana na wafuasi wa waziri mkuu wa zamani aliye gerezani Imrah Khan walioandamana kuitikia mwito wake wa kujitokeza kupinga madai ya wizi wa kura katika uchaguzi wa wiki iliyopita

https://p.dw.com/p/4cGzZ
Wafuasi wa chama cha Imrak Khan nchini Pakistan waandamana kulalamikia wizi wa kura katika matokeo ya kura za uchaguzi wa rais, mnamo Februari 11, 2024
Wafuasi wa chama cha Imrak Khan nchini Pakistan waandamana kulalamikia wizi wa kura Picha: Abdul Majeed/AFP

Duru zinasema polisi walitumia mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya waandamanaji huko Rawalpindi, Kusini mwa mji mkuu Islamabad na katika mji wa mashariki wa Lahore. Maandamano yamefanyika pia kwenye maeneo mengine bila rapsha yoyote. 

Soma pia:Wanasiasa walioungwa mkono na Khan washinda vita vya bunge Pakistan

Mwenyekiti wa chama hicho cha Tehreek-e-Insaf (PTI) Gohar Ali Khan, aliwaambia waandishi habari hapo jana kwamba vitendo vya udanganyifu kwenye uchaguzi vimefanyika kila kona ya nchi hiyo. Aliwatolea mwito wafuasi wa chama hicho kuingia mitaani leo kuonesha upinzani wao. 

Pakistan inatishiwa na mkwamo wa kisiasa

Katika uchaguzi huo ambao matokeo yake ya mwisho yametangazwa leo, wagombea binafasi wenye mafungamano na Khan wameshinda viti vingi bungeni. Lakini hawawezi kuunda serikali, hali inayotishia kuitumbukiza Pakistan kwenye mkwamo wa kisiasa wakati vyama hasimu vimeanza mazungumzo ya kujaribu kuunganisha nguvu kupata serikali ya mseto.