1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

PARIS : Waziri wa Fedha wa Ufaransa ajiuzulu

26 Februari 2005
https://p.dw.com/p/CFaw

Waziri wa Fedha wa Ufaransa Herve Gaymard amejiuzulu kutokana na kashfa ya nyumba.

Hatua hiyo inakuja kufuatia kubainika kwamba yeye, mke wake na watoto wanane walikuwa wakiishi kwenye nyumba kubwa ya kifahari mjini Paris inayolipiwa na serikali ya Ufaransa kwa gharama za Euro 14,000 kwa mwezi.

Gaymard mshirika wa Rais Jaques Chirac alikuwa ndio kwanza ameshika wadhifa huo hapo mwezi wa Novemba mwaka jana na kashfa hiyo imetokea wakati serikali ikiwa katika mpango wa kubana matumizi.