1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

PARIS: Waziri Mkuu wa Uingereza, Tony Blair, ziarani Ufaransa.

12 Mei 2007
https://p.dw.com/p/CC2x

Waziri Mkuu wa Uingereza, Tony Blair yumo ziarani nchini Ufaransa ambako ameshauriana na Rais anayeondoka, Jacques Chirac na Rais-mteule, Nicolas Sarkozy.

Mkutano huo ndio wa mwisho rasmi kati ya Tony Blair na Jacques Chirac ambaye juma lijalo atamkabidhi urais Nicolas Sarkozy.

Tony Blair ameshatangaza atang’atuka mnamo tarehe 27 mwezi ujao.

Blair alitangaza hayo saa chache baada ya kumuidhinisha Waziri wa Fedha, Gordon Brown, kuurithi uongozi wa chama tawala cha Leba na pia wadhifa wa waziri mkuu.

Gordon Brown tayari amezindua rasmi harakati zake za kuwania uongozi.