1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaSudan

Pande hasimu Sudan zatumia njaa kama silaha - Wataalamu UN

27 Juni 2024

Watalaamu wa haki za binaadamu wanaoufanyia kazi Umoja wa Mataifa wamezituhumu pande zinazozozana nchini Sudan kwa kutumia njaa kama silaha ya vita.

https://p.dw.com/p/4hawF
Zaidi ya watu milioni 11 wamelazimika kuyakimbia makaazi yao tangu mapigano ya sasa yalipoanza.
Zaidi ya watu milioni 11 wamelazimika kuyakimbia makaazi yao tangu mapigano ya sasa yalipoanza.Picha: Unamid Handout/Albert Gonzalez F/picture alliance

Kauli hiyo inatolewa wakati wasiwasi ukiongezeka kuhusiana na kuenea kwa baa la njaa nchini humo. Watalaamu hao wamesema vikosi vya jeshi la Sudan na wanamgambo wa RSF wanatumia chakula kama silaha na kuwaacha raia wateseke kwa njaa.

Wanasema kiwango cha njaa na watu kupoteza makaazi yao kinachoonekana nchini Sudan hakijawahi kushuhudiwa.

Mapigano yaliyodumu kwa miezi 14 yamewauwa zaidi ya watu 14,000 na kuwajeruhi wengine 33,000, kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, lakini wanaharakati wa haki wanasema idadi hiyo huenda ikawa juu zaidi.

Zaidi ya watu milioni 11 wamelazimika kuyakimbia makaazi yao.