1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaNicaragua

Nicaragua yawachia huru wapinzani 222 na kuwapeleka Marekani

10 Februari 2023

Serikali ya Nicaragua imewaachia huru zaidi ya wanasiasa 200 wa upinzani na kisha kuwapeleka nchini Marekani.

https://p.dw.com/p/4NJoO
Nicaragua schiebt Hunderte politische Gefangene in die USA ab
Picha: Kevin Lamarque/REUTERS

Wanasiasa hao hata hivyo wamevuliwa uraia wa Nicaragua na kupokonywa haki zote za kisiasa kwenye taifa hilo la Amerika ya Kusini.

Uamuzi huo wa kuwaachia wanasiasa hao 222 ulitangazwa ghafla na utawala wa rais Daniel Ortega wa Nicaragua ambaye analaumiwa kwa kuitumbukiza nchi hiyo kwenye mkondo wa udikteta.

Inaarifiwa uamuzi huo umefikiwa baada ya mazungumzo kati ya serikali ya Nicaragua na Marekani ambapo Washington imeridhia kuwapokea wanasiasa hao na imesema itawahudumia kwa muda wa miaka miwili.

Miongoni mwao ni Juan Sebastian Chamorro aliyetarajiwa kuchuana  na rais Ortega katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2021.

Kabla ya uchaguzi huo yeye na wenzake kadhaa walikamatwa na kuwekwa kizuizini kwenye gereza lenye ulinzi mkali.