1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaNicaragua

Nicaragua yamwaachia huru Askofu mashuhuri wa kikatoliki

15 Januari 2024

Serikali ya Nicaragua imetangaza kumwachia huru askofu mashuhuri wa kikatoliki na makasisi wengine 18 waliofungwa jela wakati wa operesheni ya kamata kamata ya rais Daniel Ortega wa nchi hiyo.

https://p.dw.com/p/4bEex
Askofu Rolando Alvarez
Askofu Rolando Alvarez wa jimbo katoliki la Matagalpa na Esteli nchini Nicaragua.Picha: Maynor Valenzuela/REUTERS

Askofu Rolando Alvarez na makasisi hao 18 walihukumiwa kifungo gerezani zaidi ya mwaka mmoja uliopita katika mfululizo wa kesi inazoaminika zilikuwa na dhima ya kuwanyamazisha viongozi wa kidini na wanasiasa wa upinzani nchini Nicaragua.

Rais Ortega aliwatuhumu wote waliokamatwa na kufungwa jela-- ikiwemo Askofu Rolando-- kwamba walikuwa waungaji mkono maandamano wa makubwa ya umma yaliyofanyika mwaka 2018 akidai yalidhamiria kuipindua serikali yake.

Kwenye taarifa yake ya usiku wa kuamkia leo, serikali ya taifa hilo la Amerika ya Kati imetangaza kuwa Askofu Rolando na wenzake wengine wameachiwa na kukabidhiwa kwa mamlaka za makao makuu ya kanisa katoliki. Taarifa ya serikali imesema taratibu zinafanyika kuwasafirisha kwenda Vatican.