1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

NEW YORK Kofi Annan amfuta kazi wa Umoja wa Mataifa

2 Juni 2005
https://p.dw.com/p/CF7k

Katibu mkuu wa umoja wa mataifa Kofi Annan, amempiga kalamu afisa wa kwanza wa umoja huo aliyehusika katika kashfa ya mpango wa mafuta kwa chakula nchini Irak, iliyouharibia sifa umoja huo.

Joseph Stephanides, ambaye amesema vitendo vyake viliidhinishwa na wakuu wake, alilisaidia kampuni moja la Uingereza kupata mkataba katika mpango huo. Amepinga kufanya makosa hayo, akisema kulikuwa na umuhimu wa kuurahakisha mpango huo kwani wairaki walikuwa wakiteseka, na ameapa atakata rufaa.