1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Nchi za G77 na China zinakutana nchini Cuba leo

Sylvia Mwehozi
15 Septemba 2023

Kundi la nchi 77 zinazoendelea na zinazoinukia la G77 na China, zimekusanyika nchini Cuba leo katika mkutano unaotafuta kukuza utaratibu mpya wa kiuchumi ulimwenguni, katikati mwa ongezeko la migawanyiko.

https://p.dw.com/p/4WMUM
Afrikareise des Kubanischen Präsidenten Díaz-Canel l Süadafrika
Rais wa Cuba Miguel Diaz-Canel,Picha: Phill Magakoe/AFP

Kundi la nchi 77 zinazoendelea na zinazoinukia la G77 na China, zimekusanyika nchini Cuba leo katika mkutano unaotafuta kukuza utaratibu mpya wa kiuchumi ulimwenguni, katikati mwa ongezeko la migawanyiko.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres, ambaye aliwasili kisiwani humo jana Alhamisi, ataungana na wakuu wa nchi na serikali  kutoka Afrika, Asia na Amerika Kusini katika mkutano wa siku mbili unaofanyika mjini Havana.

Kundi la G77 lilianzishwa mwaka 1964 na mataifa 77 kutoka nchi zinazoendelea ili kueleza na kukuza maslahi yao ya pamoja ya kiuchumi na kuongeza uwezo wa mazungumzo ya pamoja. China sio mwanachama kamili wa kundi hilo. Ijapokuwa wanachama wa kundi hilo sasa wameongezeka na kufikia 134, bado kundi hilo limesalia na jina lake la G77 ili kuzingatia historia yake.