1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Nchi tano zapata viti Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa

4 Januari 2023

Equador, Japan, Malta, Msumbiji na Uswisi, zimekaribishwa rasmi katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, zikichukua viti vyao vya miaka miwili walivyoshinda bila kupingwa mwezi Juni.

https://p.dw.com/p/4Liu3
USA UN-Sicherheitsrat
Picha: Loey Felipe/UN Photo/Xinhua/IMAGO

Balozi wa Msumbiji Pedro Comissario Afonso, ameiita kuwa siku ya kihistoria, huku Balozi wa Uswisi Pascale Baeriswyl, akisema anajisikia kuwa mwenye unyenyekevu na wajibu, wakati nchi zao zilianza mihula yao ya kwanza kabisa, kwenye taasisi hiyo yenye nguvu zaidi ya Umoja wa Mataifa.

Msumbuji ilichukua nafasi ya Kenya ambayo ilimaliza muhula wake.

Malta imejiunga kwa mara ya pili, Equador mara ya nne na Japan kwa mara ya 12. China, Ufaransa, Urusi, Uingereza na Marekani ndio wajumbe wa kudumu wenye kura ya turufu kwenye baraza hilo.