1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Nawaz Sharif arejea Pakistan baada ya miaka minne

22 Oktoba 2023

Nawaz Sharif, aliyewahi kuwa waziri mkuu mara tatu nchini Pakistan, amerejea nchini humo kuanzisha tena safari yake ya kisiasa baada ya kukimbilia uhamishoni nchini Uingereza kwa miaka minne kwa hatia ya ufisadi.

https://p.dw.com/p/4XryX
Waziri Mkuu wa zamani wa Pakistan, Nawaz Sharif, akiwa na binti yake, Maryam Nawaz, wakiwapungia wafuasi wa chama chake mjini Lahore.
Waziri Mkuu wa zamani wa Pakistan, Nawaz Sharif, akiwa na binti yake, Maryam Nawaz, wakiwapungia wafuasi wa chama chake mjini Lahore.Picha: Aamir Qureshi/AFP/Getty Images

Nawaz alirejea mjini Lahore siku ya Jumamosi (Oktoba 21) na kushiriki mkutano wa hadhara ulioandaliwa na chama chake cha Pakistan Muslim League-Nawaz (PML-N) kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Januari mwaka 2024. 

Waziri mkuu huyo wa zamani aliwaambia wafuasi wake kwamba anakutana nao kwa mara ya kwanza baada ya muda mrefu, lakini bado ana mapenzi na chama chake na wafuasi wake hawajamsaliti na hajawasaliti. 

Soma zaidi: Waziri mkuu wa zamani wa Pakistan Nawaz Sharif arejea nyumbani

Pakistan inapitia changamoto ya usalama, kudorora kwa uchumi wa taifa hilo na mgogoro wa kisiasa wakati ikijitayarisha kuandaa uchaguzi huo mkuu, huku mpinzani mkubwa wa Sharif, Imran Khan, akiendelea kufungwa jela kwa makosa ya ufisadi. 

Sharif aliyefungwa jela kwa makosa sawa na hayo, aliachiwa kutoka jela kwa dhamana mwaka 2019 kwa lengo la kupata matibabu mjini London kwa wiki sita, lakini baadaye aliamua kutorejea Pakistan kumaliza kifungo chake.