1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

NATO, G7 kuendelea kuibeba Ukraine

13 Julai 2023

Mkutano wa kilele wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Kujihami ya NATO ulimalizika Jumatano mjini Vilnius, Lithuania, ambapo miongoni mwa mambo mengine, kulijadiliwa suala la uvamizi wa Urusi dhidi Ukraine.

https://p.dw.com/p/4ToCA
Litauen | Nato-Gipfel in Vilnius | US-Präsident Joe Biden und Wolodymyr Selenskyi
Picha: Paul Ellis/AFP/Getty Images

Viongozi wa kundi la mataifa tajiri duniani, G7, na wale wa Umoja wa Ulaya wametangaza mpango wa kimataifa wa kuendelea kuisaidia Ukraine kijeshi na kuipatia uwezo mkubwa wa kuweza kujilinda na kujihami. 

Mpango huo wa kuisaidia Ukraine utajumuisha vifaa na mafunzo ya kijeshi, kubadilishana taarifa za kijasusi, na teknolojia ya ulinzi wa mtandaoni.

Soma zaidi: Mkutano wa NATO: G7 yatoa ahadi kwa Ukraine
G7 kutangaza mpango wa muda mrefu wa usalama kwa Ukraine

Rais Joe Biden wa Marekani amesema G7 itaisaidia Ukraine kuimarisha jeshi lake wakati ikisubiri kujiunga na NATO. 

Wizara ya Mambo ya Nje ya Urusi imesema hapo jana kuwa mkutano huo wa NATO unaonesha kuwa muungano huo wa kijeshi unarejea kwenye mikakati ya Vita Baridi, na kwamba Urusi itakuwa tayari kujibu vitisho kwa wakati muafaka na kwa njia inayofaa, kwa kutumia mifumo na mbinu zote walizonazo.