1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUfaransa

Mwanahabari wa Ufaransa aliyetekwa 2021 aachiwa huru Mali

21 Machi 2023

Mwandishi habari wa Kifaransa aliyetekwa nyara karibu miaka miwili iliyopita na wapiganaji wa itikadi kali katika ukanda wa Sahel ameachiwa huru.

https://p.dw.com/p/4OyEi
Screenshot aus Propagandamaterial | Entführter französischer Journalist Olivier Dubois
Picha: Social Media/AFP

Mwanahabari huyo pamoja na mfanyakazi wa misaada wa Kimarekani aliyeshikiliwa pia mateka na wanamgambo hao kwa miaka sita waliwasili jana mjini Niamey baada ya kuwachiwa huru.

Mfaransa Olivier Dubois na Mmarekani Jeffery Woodke waliwasili kwa ndege jana katika uwanja wa Niamey, mji mkuu wa Niger. Dubois mwenye umri wa miaka 48 alitekwa nyara nchini Mali mnamo Aprili 2021 wakati Woodke alitoweka nchini Niger mnamo Oktoba 2016.

Soma pia: Wafanyakazi wa Msalaba Mwekundu waliotekwa Mali, waachiwa huru

Wawili hao walizishukuru serikali za Niger, Ufaransa na Marekani kwa kushughulikia kuwachiliwa kwao. Maelezo kuhusu ni kwa nini na vipi wawili hao waliwachiwa huru hayakutolewa.