Kisa cha mwanasheria mmoja mwanamke nchini Kenya kufutwa kazi kwa kumuita mfanyakazi mwenzake wa kiume majina ya utani ambayo mwajiri aliyazingatia kuwa unyanyasaji wa kijinsia kilizusha mjadala mkali. Majina kama babe, mpenzi, darlin, cheri, husikika sana katika mahala pa kazi. Je, ni sawa au si sawa? Ungana na Bruce Amani katika Vijana Mchakamchaka.