1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mkutano wa kwanza wa mawaziri wa UAE na Israel mjini Berlin

Sekione Kitojo
6 Oktoba 2020

Waziri wa mambo ya kigeni wa Ujerumani Heiko Maas anatakuwa mwenyeji wa mkutano wa mawaziri wenzake wa Israel na Umoja wa Falme za Kiarabu UAE baada ya nchi hizo kutia saini makubaliano ya kurejesha uhusiano wa kibalozi.

https://p.dw.com/p/3jUgD
Heiko Maas | Rede per Video | UN-Vollversammlung
Picha: UNTV/AP Photo/picture-alliance

Mkutano wa pili  ni wa kansela wa  Ujerumani  Angela  Merkel na  kiongozi wa upinzani wa  Belarus Svetlana Tikhanovskaya. 

Waziri wa  mambo  ya  kigeni  wa  Ujerumani  Heiko Maas atawapokea  Gabi Ashkenazi waziri  wa mambo  ya  kigeni  wa Israel  pamoja  na  waziri wa  mambo  ya  kigeni  wa  Emirati Abdullah bin Zayed al-Nahyan mchana  wa leo.

Deutschland Israel Außenminister Heiko Maas  Gabi Ashkenazi
Waziri wa mambo ya kigeni wa Israel Gabi AshkenaziPicha: Reuters/M. Tantussi

"Ni fahari  kubwa  kwamba  mawaziri  wa  mambo  ya  kigeni  wa Israel  na  Emirati  wamechagua  Berlin  kuwa  sehemu  ya mkutano wao  wa  kwanza  wa  kihistoria," amesema  Maas  katika  taarifa kabla  ya  mkutano  huo, akiwashukuru  wenzake hao kwa  kuiamini Ujerumani.

Makubaliano "ya kijasiri  ya  amani " kati ya  Israel na  Emirati yalikuwa ni  habari nzuri za kwanza  katika  Mashariki  ya  Kati kuwahi  kutokea  kwa  muda  mrefu  na  wakati  huo  huo  ni fursa  ya vuguvugu  jipya  katika  majadiliano  kati ya  Waisraeli na Wapalestina , amesema.

Maas  ana matumaini , "kwamba  Berlin  itatoa  fursa  nzuri  kwa hatua  zaidi  za  majadiliano  katika  mwelekeo  huo."

Außenminister Vereinigte Arabische Emirate Al Nahyan
Waziri wa mambo ya kigeni wa UAE Abdullah bin Zayed al-Nahyan Picha: JACQUES DEMARTHON/AFP/Getty Images

Mkutano  huo  unakuja  baada  ya  mawaziri  wa  mambo  ya  kigeni wa  UAE  na  Bahrain  kukamilisha  uanzishwaji  wa  mahusiano  ya kibalozi  na  waziri  mkuu  wa  Israel  Benjamin  Netanyahu  hapo Septemba  15.

Tikhanovskaya

Utiaji  saini  ulifanyika  mbele  ya  rais  wa  Marekani Donald Trump katika  ikulu  ya  White House  mjini  Washington.

Kwa upande  wake  kansela  wa  Ujerumani  Angela  Merkel anatarajiwa  kukutana  na  kiongozi  wa  upinzani  nchini  Belarus Svetlana  Tikhanovskaya. Akizungumza  na  gazeti la  Der Spiegel kabla  ya  mkutano  huo, Tikhanovskaya  alionesha  kuwa majadiliano  yanaweza  kujumuisha  uwezekano wa  kansela  kufanya upatanishi  katika  mzozo huo  nchini  mwake.

Rais  wa  muda  mrefu  wa  Belarus Alexander Lukashenko anaendelea  kuwa  madarakani  mjini  Minsk  licha  ya  kukataliwa  na Ujerumani na  mataifa  mengi mengine  katika  uchaguzi  wa  hapo Agosti, ambapo  alidai  kupata  ushindi  wa  kishindo.

Tikhanovskaya alikuwa  wa  pili  katika uchaguzi  huo, kwa mujibu wa matokeo  rasmi  ya  jumla.

Schweiz Genf UN Swetlana Tichanowskaja Oppositionsführerin Belarus
Kiongozi wa upinzani nchini Belarus Svetlana TikhanovskayaPicha: Fabrice Coffrini/AFP/Getty Images

Waungaji wake mkono  wanadai  kuwa  ameshinda  uchaguzi huo. Msemaji  wa  Merkel, Steffen Seibert , amesema  kansela anasubiri kwa  hamu  mkutano  huo  na  amesisitiza  uungaji  mkono  wa Ujerumani  wa maandamano  ya  amani  ya  kupinga  serikali  nchini Belarus.

mara baada ya  kukutana  na  Merkel , Tikhanovskaya  anatarajiwa kukutana  na  viongozi  wa  vyama  vya  Green mjini  Berlin. Kesho Jumatano anatarajiwa  kukutana  na  waziri  wa  mambo  ya  kigeni Heiko Maas.