1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mkutano wa kilele wa BRICS kuanza nchini Afrika Kusini

22 Agosti 2023

Mkutano wa kilele wa kundi la mataifa yanayoinukia kwa kasi kiuchumi la BRICS unaanza leo Jumanne nchini Afrika Kusini chini ya kauli mbiu ya "BRICS na Afrika".

https://p.dw.com/p/4VQUD
Kauli mbiu ya mkutano huo wa kilele unaoanyika Afrika Kusini ni: "BRICS na Afrika".
Kauli mbiu ya mkutano huo wa kilele unaoanyika Afrika Kusini ni: "BRICS na Afrika".Picha: MARCO LONGARI/AFP

Ajenda kubwa ya mkutano huo wa 15 ni kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia na kiuchumi kati ya kundi hilo na bara la Afrika na uwezekano wa kupokea wanachama zaidi katika siku zijazo.

Kundi hilo linaloyajumuisha mataifa ya Brazil, Urusi, India, China na mwenyeji Afrika Kusini linatizamwa kuwa mbadala kwa udhibiti mkubwa sekta za uchumi na fedha duniani ulio chini ya mataifa ya magharibi.

Mkutano huo utakaoendelea hadi siku ya Alhamisi mjini Johannesburg, unahudhuriwa na viongozi wote wa kundi hilo isipokuwa rais Vladimir Putin wa Urusi ambaye atashiriki kwa njia ya video.

Putin anayetakiwa na mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC atawakilishwa na waziri wake wa mambo ya kigeni Sergei Lavrov.