1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Miito ya usitishaji vita Gaza yaendea kutolewa

23 Februari 2024

Maafisa wa wizara ya Afya ya Gaza inayosimamiwa na wanamgambo wa Hamas wamesema mashambulizi ya Israel yamewaua watu 71 kusini mwa ukanda huo jana Alhamisi.

https://p.dw.com/p/4cn0T
Ukanda wa Gaza | Uharibifu katika Rafah
Uharibifu katika RafahPicha: Hatem Ali/AP Photo/picture alliance

Hayo yameripotiwa wakati kiongozi wa kisiasa wa kundi la Hamas Ismail Haniyeh ameondoka Misri baada ya kufanya mazungumzo na maafisa wa taifa hilo kuhusu uwezekano wa makubaliano ya usitishaji vita kwa ubadilishanaji wa mateka wa Israel walioko mikononi mwao na wafungwa wa Palestina walioko magereza ya Israel kuachiliwa huru.

Wanadiplomasia wa Ulaya wamezidisha miito yao ya kutaka mapigano yasitishwe  kama tahadhari dhidi ya mzozo wa kibinadamu unaozidi kuwa mbaya Ukanda wa Gaza.

Vita vya Gaza vilianza baada ya Hamas kufanya shambulizi baya kusini mwa Israel na kuua watu 1,200 na kuwashika mateka wengine 250.

Israel, Marekani, Umoja wa Ulaya miongoni mwa mataifa mengine huliorodhesha Hamas kuwa kundi la kigaidi.