1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroIsrael

Mateka 10 zaidi wa Israel waachiwa huru

29 Novemba 2023

Kundi la Hamas limewaachia huru mateka wengine 10 wa Israel pamoja na raia wawili wa Thailand ikiwa ni sehemu ya utekelezaji mkataba wa kusitisha mapigano uliorefushwa kwa muda siku mbili.

https://p.dw.com/p/4ZYdK
Mzozo wa Israel na Hamas | Mateka
Waisraeli waliochukuliwa mateka na kundi la Hamas wakiwa njiani kwenda kukabidhiwa kwa mamlaka za Israel.Picha: Hamas Military Wing/Handout via REUTERS

Shirika la Msalabaa Mwekundu limethibitisha kupokea kundi hilo la mateka na kuwakabidhi kwa mamlaka za Israel. Miongoni mwao ni wanawake 9 na msichana mmoja mwenye umri wa miaka 17.

Kwa upande wake Israel nayo imewaachia huru wafungwa 30 wa Kipalestina waliokuwa wakishikiliwa kwenye moja ya jela zake.

Israel na kundi la Hamas walikubaliana kurefusha muda wa kusitisha mapigano kwa siku mbili zaidi kuanzia jana baada ya kumalizika kwa awamu ya kwanza ya siku nne.

Tangu usitishaji mapigano ulipoanza Ijumaa iliyopita, kundi la Hamas limewaachia huru jumla ya mateka 81, wengi wakiwa raia wa Israel na mamlaka za Israel zimewatoa jela Wapalestina 180.